| Index 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71 72 73 74 75 76 77 78 79 80 81 82 83 [84] 85 86 87 88 89 90 91 92 93 94 95 96 97 98 99 100 101 102 103 104 105 106 107 108 109 110 111 112 113 114 |
|
[84.1] Itapo chanika mbingu, [84.2] Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza, [84.3] Na ardhi itakapo tanuliwa, [84.4] Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu, [84.5] Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza, [84.6] Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta. [84.7] Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia, [84.8] Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi, [84.9] Na arudi kwa ahali zake na furaha. [84.10] Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake, [84.11] Basi huyo ataomba kuteketea. [84.12] Na ataingia Motoni. [84.13] Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake. [84.14] Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena. [84.15] Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona! [84.16] Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa, [84.17] Na kwa usiku na unavyo vikusanya, [84.18] Na kwa mwezi unapo pevuka, [84.19] Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka! [84.20] Basi wana nini hawaamini? [84.21] Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu? [84.22] Bali walio kufuru wanakanusha tu. [84.23] Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria. [84.24] Basi wabashirie adhabu chungu! [84.25] Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika. |